Psalms 106:1-6
Wema Wa Bwana Kwa Watu Wake
1 aMsifuni Bwana.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.
2 bNi nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana
au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 cHeri wale wanaodumisha haki,
ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 dEe Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako,
uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 eili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako,
niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako,
na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 fTumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda,
tumekosa na tumetenda uovu.
Copyright information for
SwhKC