Psalms 106:1-6

Wema Wa Bwana Kwa Watu Wake


1 aMsifuni Bwana.

Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.

2 bNi nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana
au kutangaza kikamilifu sifa zake?

3 cHeri wale wanaodumisha haki,
ambao daima wanafanya yaliyo mema.

4 dEe Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako,
uwe msaada wangu unapowaokoa,

5 eili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako,
niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako,
na kuungana na urithi wako katika kukusifu.


6 fTumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda,
tumekosa na tumetenda uovu.
Copyright information for SwhKC